NA MWANDISHI WETU,ZANZIBAR
OFISA Utawala wa Wakala wa Uagizaji Mafuta kwa Pamoja (PBPA),Bertha Mganga ametoa elimu kuhusu majukumu na shughuli za Wakala kwa wananchi waliotembelea banda la PBPA katika Tamasha la Kizimkazi 2026, linalofanyika Dimbani, Kizimkazi, Zanzibar.
Tamasha hilo limefunguliwa rasmi leo, Agosti 12, 2026, na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Dk. Hussein Ali Mwinyi.




