BRAZIL
Chama cha soka Brazil kinafikiria kumpa kazi ya quinoa time yao ya taifa meneja wa zamani wa time ya taifa ya Hispania na Barcelona, Luis Enrique kuchukua nafasi ya Tite aliyejiuzulu baada ya Brazil kuondolewa kwenye kombe la dunda 2022.
LIVERPOOL

Liverpool wapo mbioni kuwasajili viungo Ryan Gravenberch anayekipiga Bayern Munich na Uholanzi pamoja na Jude Bellingham wa England na Borussia Dortmund ili waimarishe scheme ya kiungo inayoonekana kupwaya.
LA GALAXY

Baada ya mpango wao wa kumchukua kwa mkopo kugonga mwamba, LA Galaxy wameonyesha nia ya kumsajili jumla kiungo wa kati wa Chelsea, Mbrazil Andrey Santos.
AS ROMA

Licha ya yeye mwenyewe kusema anatamani kuendelea kubaki AS Roma, mlinzi wa zamanı wa Manchester United, Chris Smalling anawaniwa na klabu za Fulham, Everton, Leicester na West Ham.
LIVERPOOL

Liverpool, Newcastle, Tottenham na West Ham ni miongoni mwa klabu za Ligi Kuu Uingereza zinazohitaji huduma ya kiungo wa kati wa Mainz na Ujerumani, Anton Stach.
CHELSEA

Mshambuliaji wa Ureno na Atletico Madrid anayekipiga kwa mkopo kwenye klabu ya Chelsea, Joao Felix, 23, anataka mpataba wake uwe wa kudumu Chelsea.