Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dk Emmanuel John Nchimbi, akizungumza na watumishi wa CCM Makao Makuu pamoja na jumuiya zake, Jumuiya ya Wazazi, Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM) na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), kwenye Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM (NEC), Dodoma, Jumanne, Februari 6, 2024. Wengine meza kuu, ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM – Bara, Anamringi Macha na Katibu wa NEC, Fedha na Uchumi, Dk.Frank Haule.Baadhi ya Watumishi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Makao Makuu, pamoja na jumuiya zake, Umoja wa Wazazi, Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), na Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT), wakimsikikiza na kufuatilia kwa makini hotuba ya Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, wakati wa kikao na watumishi hao, katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa (NEC), jijini Dodoma, Jumanne, Februari 6, 2024.